C - NEWS

Alikiba Kuachia EP Yake ya Kwanza ‘STARTER’

Alikiba Kuachia EP Yake ya Kwanza 'STARTER'

Alikiba, mfalme wa muziki wa Bongo Flava, anatangaza kuachia Extended Playlist (EP) yake ya kwanza iitwayo “STARTER The EP,” ambayo itatolewa rasmi Ijumaa, tarehe 20 Septemba 2024 kupitia lebo ya Kings Music Records.

RELATED: Alikiba Ft Billnass – Fallen Angel

EP hii itakuwa na jumla ya nyimbo 7, ikiwa ni pamoja na kolabo na wasanii maarufu kama Nandy, Marioo, na Jay Melody. Watayarishaji wakubwa kama Cukie, Mafeeling, Mocco Genius, GeniusJini, na O, Right wamehusika katika kuunda EP hii, ikionyesha mwelekeo mpya wa muziki wa Alikiba.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Alikiba amewahamasisha mashabiki wake kwa kujivunia ladha halisi ya Bongo Flava ambayo inamfanya kuwa mmoja wa wasanii wakubwa nchini Tanzania. Mashabiki wa Bongo Flava kote ulimwenguni wanangojea kwa hamu kuona jinsi EP hii itakavyokuwa na kuleta msisimko mpya katika tasnia.

Hapa kuna orodha ya nyimbo kwenye EP ya Alikiba “STARTER The EP”:

  1. Alikiba – Nahodha
  2. Alikiba – Top Notch Ft Marioo
  3. Alikiba – Kheri
  4. Alikiba – Hatari Ft Jay Melody
  5. Alikiba – Bailando Ft Nandy
  6. Alikiba – Chibaba
  7. Alikiba – Nahodha Acoustic

RELATED: Alikiba – Yalaiti Ft Sabah Salum

Also, check more tracks from Alikiba;

Leave a Comment