ENTERTAINMENT

TANZANIA: Wagonjwa wa Corona wafika 46, Baada ya wengine 14 Kuongezeka

Habari iliyotufikia hivi punde ni kwamba Wagonjwa wa Corona wafika 46 huko nchini Tanzania, ni baada ya wagonjwa wengine 14 kuongezeka.

Wizara ya Afya Maendeleo ya jamii jinsia na watoto leo tarehe 13 April imeripoti ongezeko la wagonjwa wapya 14 wa ugonjw wa Covid 19 nchini

Katika Taarifa iliyotolewa leo wizara imesema wagonjwa wote ni watanzania na 13 kati yao wapo mkoani Dar es salaam na mmoja yupo mkoni Arusha.

Ongezeko la wagonjwa hao wapya 14 linaongeza idadi ya jumla ya wagonjwa kufikia 46 kutoka 32 ya siku kadhaa zilizopita

Mpaka sasa Tanzanai imesharipoti vifo vitatu vinavyosababishwa na ugonjwa huu.

Leave a Comment